Biden na Putin kukutana mjini Geneva

0


Rais Joe Biden wa Marekani na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin wanakutana leo Jumatano mjini Geneva kwa mazungumzo ya kwanza ambayo hayabebi matumaini makubwa ya kumaliza tofauti zilizopo kati ya Washington na Moscow.

Wakiwa njiani kuelekea mjini Geneva, afisa mmoja mwandamizi wa serikali ya Marekani amesema hawana matarajio ya kupatikana mafanikio makubwa kwenye mkutano huo kati ya Biden na Putin utakaofanyika kwa muda saa tano.

Matamshi sawa na hayo yametolewa pia na mshauri wa sera za kigeni wa rais Putin, Yuri Ushakov ambaye amesema hakuna uwezekano wa kufikiwa makubaliano yoyote kwenye mkutano huo.

Hata hivyo pande zote mbili zimesema mazungumzo baina ya viongozi hao wawili ni muhimu kuelekea mahusiano thabiti na yanayotabirika kati ya Washington na Moscow ambazo zimeshuhudia mahusiano yakitetereka hadi kiwango cha chini kabisa miaka ya karibuni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable