DRC: Kiongozi wa kivita katika Hifadhi ya Virunga akamatwa

0
Walinda mazingira katika Hifadhi ya Virunga wakipiga doria. (picha ya kumbukumbu)
Walinda mazingira katika Hifadhi ya Virunga wakipiga doria. (picha ya kumbukumbu) Virunga National Park/AFP/File
Ujumbe kutoka:RFI
Jackson Muhukambuto alikamatwa mapema wiki hii nje kidogo ya mji wa Butembo. Ilichukuwa miezi sita ili Walinzi wa mazingira wafanikiwe kumkamata, amesema mkurugenzi wa Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga. Kulingana na Emmanuel de Merode, Jackson Muhukambuto na kundi lake la wanamgambo, Mai Mai Jackson, wanashukiwa kuhusika katika mauaji kadhaa.

Katika kipindi cha miaka mitatu, inasemekana waliwaua walinzi wa mazingira kumi na tisa, raia wengi pamoja na wanajeshi kadhaa.

Jackson Muhukambuto ambaye ni mto katika jeshi la FARDC na mpiganaji wa zamani katika makundi kadhaa ya waasi, anaongoza kundi lenye silaha linalotekeleza uhalifu wake katika eneo linalokadiriwa kuwa zaidi ya nusu ya Hifadhii ya Virunga. Hifadhi inayopima kilomita mraba 7,800.

Jackson Muhukambuto anasemekana kuwa na mitandao yenye nguvu ndani ya jeshi na kati ya wafanyabiashara katika jamii ya Nande, ripoti ya hivi karibuni kuhusu hali ya makundi yenye silaha mashariki mwa DRC ilisema.

Kulingana na vyanzo vya kutokaHifadhi ya Viunga, kukamatwa kwa Muhukambuto kulikuja baada ya kurushiana risasi kati ya wapiganaji wake na walinzi wa mazingira.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable