
Katika kipindi cha miaka mitatu, inasemekana waliwaua walinzi wa mazingira kumi na tisa, raia wengi pamoja na wanajeshi kadhaa.
Jackson Muhukambuto ambaye ni mto katika jeshi la FARDC na mpiganaji wa zamani katika makundi kadhaa ya waasi, anaongoza kundi lenye silaha linalotekeleza uhalifu wake katika eneo linalokadiriwa kuwa zaidi ya nusu ya Hifadhii ya Virunga. Hifadhi inayopima kilomita mraba 7,800.
Jackson Muhukambuto anasemekana kuwa na mitandao yenye nguvu ndani ya jeshi na kati ya wafanyabiashara katika jamii ya Nande, ripoti ya hivi karibuni kuhusu hali ya makundi yenye silaha mashariki mwa DRC ilisema.
Kulingana na vyanzo vya kutokaHifadhi ya Viunga, kukamatwa kwa Muhukambuto kulikuja baada ya kurushiana risasi kati ya wapiganaji wake na walinzi wa mazingira.