Familia ya Uingereza inayosema ina undugu wa damu na rais wa Marekani

0


Familia ya Uingereza inayosema ina undugu wa damu na rais wa Marekani

Paul Hariss, binti yake Rose Pattonn awatoto wake
Image caption: Paul Hariss, binti yake Rose Pattonn watoto wake

Wiki iliyopita, BBC ilichunguza madai kuwa Rais wa Marekani Joe Biden ana uhusiano kijeni na England. Tangu wakati huo, familia moja ya England imejitokeza na kusema ni ndugu wa rais Biden.

Kwa miaka 20 Paul Harris, amekua akifanya uchunguzi wa historia yake. Aliweza kukusanya taarifa kuhusu nasaba.

Alijifunza mengi kutoka kwa bibi (nyanya)yake , Kathleen Mary Brooks, na mama yake Ann Maria Davies.

Ilijitokeza kwamba jina la Biden lilitoka kwenye familia yake . Lakini hakulitilia maanani sana suala hilo hadi siku moja mwaka jana ambapo binti yake Rose Patton ghafla aliposema.

"Si itakuwa jambo zuri kama tukiwa ndugu wa Joe Biden?" alisema Rose, akimaanisha rais mpya aliyechaguliwa Marekani.

Harris alishangazwa na kauli hiyo na ndipo alipoanza kufuatilia suala hilo. Uchunguzi wake ulibaini uhusiano wa nguvu baina ya rais Biden na ndugu zake walioishi Westbourne, kijiji kilichopo West Sussex, England.

Harris, mwenye umri wa miaka a 60 – mtengenezaji wa programu za kompyuta, anadai rais wa Marekani ana undugu na bibi yake wa tatu Emily Biden.

Aliishi katika Westbourne, ambako vizazi kadhaa vya familia yake viliishi . Watu wa famialia yake walikuwa ni pamoja na mjomba wake William Biden,ambaye anaaminiwa kuwa alihamia nchini Marekani katika miaka ya mwanzoni 1800.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable