India yatuma zaidi ya wanajeshi 50,000 kwenye mpaka China

0


India imepeleka zaidi ya wanajeshi 50,000 kwenye eneo la mpaka wake na China katika miezi ya hivi karibuni.

Kulingana na taarifa za Bloomberg, chombo cha habari kilichokuwa na makao yake makuu nchini Marekani,  maafisa 4 wa India walinukuliwa wakisema kwamba India imetuma wanajeshi wasiopungua elfu 50 kwa mikoa mitatu ya Jammu Kashmir na Wilaya ya Umoja wa Ladak kaskazini magharibi mwa nchi katika miezi ya hivi karibuni.

Maafisa hao walieleza kuwa pamoja na wanajeshi, vikosi vya silaha kali na ndege za kivita pia zilitumwa kwa mkoa huo.

Wawili kati ya maafisa hao walisema kwamba India kwa sasa ina zaidi ya vitengo 450,000 vya kijeshi, pamoja na vikosi vya jeshi vinavyojumuisha karibia wanajeshi 200,000 maeneo ya mpaka wa China.

Wakati mamlaka ilionya kuwa upotovu wowote unaweza kusababisha mzozo kati ya nchi hizo mbili, jeshi la India bado halijatoa taarifa rasmi juu ya suala hilo.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable