Jaji Mkuu mwingine wa zamani Kenya amkosoa Rais Kenyatta

0

Jaji Mkuu mwingine wa zamani Kenya amkosoa Rais Kenyatta

David Maraga
Image caption: Jaji Mkuu wa zamani wa Kenya David Maraga

Hatua ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuwakataa majaji sita waliopendekezwa na Tume ya Hudama za Mahakama,JSC, imeendelea kuzua hisia mseto.

Kiongozi wa hivi punde kutoa kauli yake kuhusiana na suala hilo ni Jaji Mkuu mshaafu David Maraga.

Katika mahojiano na Kituo cha Televisheni cha KTN, Bwana Maraga alisema: ''Hali kama hii ikiendelea nchini itaongozwa bila katiba''

Maraga amemtaka rais Kenyatta kuwateua majaji sita aliowaacha nje.

''Muda umewadia kwa bunge kumuondoa madarakani (Uhuru) akikiuka katiba'' aliongeza kusema.

Majaji hao sita ni miongoni mwa majaji 41 ambao walikuwa wamependekezwa kwa ajili ya uteuzi na Tume ya Huduma za mahakama nchini humo (JSC) miaka miwili iliyopita. Mmoja wa majaji hao alifariki.

Rais Kenyatta amekataa mapendekezo ya JSC licha ya maagizo mawili ya mahakama yaliyomtaka kufanya hivyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable