Kasisi akamatwa kwa kuwashambulia maaskofu kwa tindikali

0


Kasisi mmoja amekamatwa mjini Athens baada ya kuwasahambulia maaskofu saba wa kanisa la Othodox nchini Ugiriki, polisi wanasema.

Shambulio hilo lilitokea wakati wa kikao cha nidhamu dhidi ya kasisi huyo mwenye umri wa miaka 36 siku ya Jumatano, kulingana na polisi.

Maaskofu hao watatu waliochomeka vibaya hasa usoni wanapokea matibabu hospitalini.

Polisi aliyejaribu kuwasaidia pia alikimbizwa hospitali.

Mshukiwa, kasisi ambaye anakabiliwa na hatari ya kufurushwa kutoka kwa kanisa hilo, alituhumiwa kw akuhusika na ulanguzi wa dawa za kulevya, kwa mujibu wa shirika la habari la ANA.

Maaskofu walikuwa wanakutana kujadili mienendo yake baada ya kudaiwa kupatikana na gramu 1.8 ya dawa ya kulevya aina ya cocaine mwezi Juni 2018, kulingana na vyambo vya habari nchini Ugiriki.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable