Mahakama nchini Uswizi leo inatarajiwa kutoa uamuzi wa kesi inayomkabili kamanda wa zamani wa waasi huko Liberia.
Alieu Kosiah anatuhumiwa kwa kutekeleza makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu ikiwemo ubakaji na mauaji kati ya mwaka 1993 na 1996, wakati wa vita vya muda mrefu vya wenyewe kwa wenyewe. Amekana mashtaka hayo.
Bw. Kosiah aliyekimbilia nchini Uswizi kwa zaidi ya miaka 20 iliyopita alikamatwa mwaka 2014.
Ni raia wa kwanza wa Liberia kushtakiwa kwa uhalifu wa kivita unaohusiana na mzozo huo.
