Kiongozi wa Sudan aonya juu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe na kutetea mageuzi

0




Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok, ameonya kwamba nchi hiyo huenda ikatumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuwaelekezea kidole cha lawama wandani wa karibu wa utawala uliopita.

Amesema marekebisho ambayo amekuwa akitekeleza yalilenga kuboresha uchumi

Kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta imesababisha maandamano kote nchini.

"Kuzorota kwa hali ya usalama kunahusishwa sana na mgawanyiko uliokumba masuala yaliyofikiwa wakati wa mapinduzi, ambayo yaliacha ombwe linalotumiwa na maadui zake na wafuasi wa serikali ya zamani'', Bw. Hamdok alinukuliwa na shirika la Reuters.

Sudan imepongezwa kwa mageuzi yake ya kiuchumi tangu rais wa zamani Omar al-Bashir alipong’olewa madarakani mwaka 2019.

Hata hivyo kumekuwa na upungufu wa chakula unaohusishwa na mizozo ya muda mrefu na majanga ya asili kama ukame na njaa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable