Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok, ameonya kwamba nchi hiyo huenda ikatumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuwaelekezea kidole cha lawama wandani wa karibu wa utawala uliopita.
Amesema marekebisho ambayo amekuwa akitekeleza yalilenga kuboresha uchumi
Kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta imesababisha maandamano kote nchini.
"Kuzorota kwa hali ya usalama kunahusishwa sana na mgawanyiko uliokumba masuala yaliyofikiwa wakati wa mapinduzi, ambayo yaliacha ombwe linalotumiwa na maadui zake na wafuasi wa serikali ya zamani'', Bw. Hamdok alinukuliwa na shirika la Reuters.
Sudan imepongezwa kwa mageuzi yake ya kiuchumi tangu rais wa zamani Omar al-Bashir alipong’olewa madarakani mwaka 2019.
Hata hivyo kumekuwa na upungufu wa chakula unaohusishwa na mizozo ya muda mrefu na majanga ya asili kama ukame na njaa.

