
Wapiganaji wa Kiisilamu Jumanne jioni walishambulia kambi ambayo ilikuwa ikitumiwa kama hifadhi kwa wafanyakazi hawa, katika mkoa wa Baghlan, kaskazini mwa Afghanistan, eneo lililokabiliwa na mapigano makali katika wiki za hivi karibuni.
"Taliban waliwachukua na kuwapeleka katika chumba kimoja na kuwafyatulia risasi," ameema msemaji wa polisi wa mkoa huo Jawed Basharat, ambaye pia aliripoti majeruhi 14.
Jawed Basharat amebaini kwamba wahanga walikuwa wakifanya kazi katika shirika la Halo Trust, shirika kuu linalojihusisha katika juhudi za kuondoa mabomu na vifaa vingine vya kulipuka vinavyoripotiwa nchini kote Afghanistan baada ya miongo kadhaa ya mizozo.
Mapigano kati ya vikosi vya Taliban na serikali yameongezeka na yameenea katika majimbo 26 kati ya 34 ya Afghanistan tangu Marekani ilipotangaza mwezi wa Aprili kuwa itaondoa wanajeshi wake Septemba 11, maafisa wanasema.