Mkutano wa pili wa Berlin kuhusu Libya waanza

0


Mkutano wa Pili wa Berlin kuhusu Libya ulianza kwa ushiriki wa wahusika wa kimataifa, pamoja na Uturuki, chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa na Ujerumani.

Mchakato wa kisiasa nchini Libya na uchaguzi wa Desemba 24 unatarajiwa kujadiliwa katika Mkutano wa pili wa Berlin, ambapo Uturuki inawakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje Mevlüt Çavuşoğlu.

Waziri Mkuu wa Libya Abdulhamid Dbeibeh, katika ujumbe aliochapisha kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter kuhusu mkutano huo alisema,

"Tunakataa kurudi kwenye vita na kuchezea mustakabali wa serikali. Tutafanya kila juhudi kuhakikisha ustawi wa watu wetu na utulivu wa nchi yetu."

Waziri Mkuu wa Libya alibainisha kuwa alikuwa huko Berlin "kutimiza upya ahadi zilizotolewa na washiriki katika Mkutano wa Kwanza wa Berlin na kuunga mkono utulivu wa Libya, uadilifu wa ardhi na umoja, na pia kushirikiana na marafiki wa Libya juu ya suluhisho la ulinzi wa watu na taifa kwa ujumla. "

Akizungumzia uchaguzi uliopangwa kufanyika Desemba, Dbeibeh pia alisema:

"Kuna changamoto nyingi mbele, lakini tuna fursa kubwa ya kufanikisha demokrasia na kuwapa watu wa Libya ujasiri wa kuchagua mwakilishi wao kupitia uchaguzi huru na wa haki."

Dbeibeh alimalizia kusema kuwa "katika hatua hii muhimu ya historia ya Libya, ni vyema kuiunganisha jamii ya kimataifa na kuhakikisha kuwa sauti ya watu wa Libya inasikika."

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable