Mkuu wa mkoa aliyetaka wananchi wabebe mabango kumkaribisha rais mashakani

0


Mkuu wa mkoa aliyetaka wananchi wabebe mabango kumkaribisha rais mashakani

Rais Samia Suluhu

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Albert Chalamila leo Juni 11, 2021.

Chalamila amedumu kwenye nafasi hiyo kwenye mkoa wa Mwanza kwa siku 23 tu baada ya kuapishwa na Rais Samia Mei 19 mwaka huu baada ya kuhudumu kama mkuu wa mkoa wa Mwanza.

Rais Samia amechukua hatua hiyo siku mbili kabla ya kuanza ziara yake ya siku tatu katika mkoa huo, ambapo pamoja na mambo mengine anatarajiwa kuzungumza na maelfu ya vijana kama alivyofanya wiki hii alipozunguza na maelfu ya wanawake mkoani Dodoma.

Chalamila alikuwa anasifika kwa kutoa kauli tata hasa anapokuwa kwenye mijumuiko ya utekelezaji wa majukumu yake, tangu akiwa katika nafasi ya ukuu wa wilaya na baadae mkuu wa mkoa wa Mbeya.

Siku mbili zilizopita Chalamila aliwataka wananchi wa mkoa wa Mwanza, wabebe mabango na kwenda nayo kwenye ziara ya Rais Samia hata kama yana ‘matusi’, kauli ambayo wengi wanaitafsiri kama ndiyo sababu ya kuondolewa kwake. huu.

Ingawa hakuna uthibitisho wa hilo, lakini kauli hiyo inapingana na maagizo ya Rais aliyoyatoa hivi karibuni, akisema kwenye ziara yake mikoani akikuta mabango yoyote yamebebwa na wananchi, basi viongozi husika wa eneo hilo watawajibika ikiwemo kufutwa kazi.

Hata hivyo Chalamila katika malezo yake ya awali kuhusu ziara ya Rais Samia mkoani Mwanza, alisema kauli ya Rais ilimaanisha mabango mengine, lakini mabango yenye nia njema hayajakatazwa kwa faida ya utatuzi wa jambo ama masuala ya maendeleo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable