UN yataka usalama kuimarishwa DRC baada ya watu 19 kuuawa

0

 

Uvamizi wa mara kwa mara unafanywa katika mkoa wa mashariki na kikundi cha waasi
Image caption: Uvamizi wa mara kwa mara unafanywa katika mkoa wa mashariki na kikundi cha waasi

Watu 19 wameuawa katika msururu wa mauaji nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Madaktari wasiokua na mipaka au Médecins Sans Frontières wamesema raia 10 waliuawa baada ya hospitali kushambuliwa katika mji wa Boga mashariki mwa DRC siku ya Jumatatu.

Miili kadha iliripotiwa kupatikana baada ya wakulima kushambuliwa katika mpaka kati ya mikoa ya Kivu Kaskazini na Ituri.

Mashambulio ya mara kwa mara yamekuwa yakifanywa katika eneo hilo na Vikosi vya Allied Democratic au ADF– moja ya makumi ya makundi yaliyojihami mashariki mwa DRC.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable