Watu 19 wameuawa katika msururu wa mauaji nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Madaktari wasiokua na mipaka au Médecins Sans Frontières wamesema raia 10 waliuawa baada ya hospitali kushambuliwa katika mji wa Boga mashariki mwa DRC siku ya Jumatatu.
Miili kadha iliripotiwa kupatikana baada ya wakulima kushambuliwa katika mpaka kati ya mikoa ya Kivu Kaskazini na Ituri.
Mashambulio ya mara kwa mara yamekuwa yakifanywa katika eneo hilo na Vikosi vya Allied Democratic au ADF– moja ya makumi ya makundi yaliyojihami mashariki mwa DRC.
