Wanamgambo 14 walinaswa katika operesheni iliyoendeshwa dhidi ya shirika la kigaidi la Al-Shabaab nchini Somalia.
Kulingana na taarifa katika vyombo vya habari vya nchi hiyo, Jeshi la Kitaifa la Somalia (SNA) liliendesha operesheni dhidi ya shirika hilo katika eneo la Middle Shabel nchini humo.
Risasi za kijeshi na silaha za wanachama wa shirika zilikamatwa kwenye operesheni hiyo ambayo wanamgambo 14 wa Al-Shabaab walikamatwa.
Shirika la Al-Shabaab mara nyingi hufanya mashambulizi yakilenga vikosi vya usalama na makazi ya raia nchini Somalia.
Katika nchi ya Somalia ambayo inajiandaa kwa uchaguzi ulioahirishwa, operesheni za jeshi dhidi ya Al-Shabaab bado zinaendelea. Katika siku za hivi karibuni, karibu wanamgambo 300 wa shirika hilo waliweza kuangamizwa katika operesheni zilizotekelezwa.
