Imeripotiwa kuwa raia wasiopungua 20 wamepoteza maisha katika mashambulizi ya shirika la kigaidi la Al-Shabaab dhidi ya raia nchini Somalia.
Mohammed Mahmud, naibu mkuu wa polisi katika Wilaya ya Galmudug, ameripoti kuwa raia wasiopungua 20 wameuawa wakati magaidi walipofyatua risasi baada ya shambulizi la kujitoa muhanga.
Al-Shabaab imedai kuwa imewaua wanajeshi wasiopungua 34 katika mashambulizi hayo.
Shirika la kigaidi la Al Shabaab mara nyingi huandaa mashambulizi yakilenga vikosi vya usalama na makazi ya raia nchini.
Operesheni za jeshi zinaendelea nchini humo ambapo uchaguzi unatarajiwa kufanyika hivi karibuni.
