Kutokana na kuongezeka kwa shida za kiusalama kaskazini mwa nchi, Nigeria imeamua kupiga marufuku sherehe za Eid al-Adha (Julai 19-21).
Katika taarifa iliyoandikwa, Msemaji wa Utawala wa Katsina Iro Bindawa alisema kuwa kwa sababu ya shida za kiusalama nchini, baadhi ya mikoa ikiwa ni pamoja na Utawala wa Daura wa Katsina, hakutafanywa sherehe za Eid mwaka huu.
Bindawa alisema kuwa hafla za farasi, ambazo hufanyika kila mwaka na Utawala wa Daura ni marufuku mwaka huu.
Bindawa alitoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kuchukulia likizo hiyo kama fursa ya kuombea amani nchini.
"Serikali inajali usalama wa watu, kwa hivyo kila mtu anaombwa kukaa nyumbani wakati wa likizo" alitumia kifungu cha maneno hayo.
Kama matokeo ya kuongezeka kwa shida za kiusalama nchini Nigeria, watu 21 waliuawa kwenye shambulizi la watu wenye silaha katika jimbo la Katsina mnamo Julai 6.
Nigeria, nchi yenye idadi kubwa zaidi ya watu barani Afrika ambayo ni takriban milioni 200, ina idadi kubwa zaidi ya Waislamu Afrika Magharibi.
Nchi hiyo ambapo Waislamu wanaunda zaidi ya nusu ya idadi ya watu, shughuli anuwai kama vile halfa za farasi hufanyika kila mwaka wakati wa sherehe za sikukuu ya Eid.
