Kampuni kubwa ya kiteknolojia ya Marekani Apple imekuwa kampuni ya kwanza kupata hesabu ya soko la hisa ya $3tn (£2.2tn).
Bei ya hisa za kampuni hiyi ilipanda kwa karibu asilimia The firm's share price has 5,800 tangu mwanzilishi mwenza na mtendaji mkuu wa zamani Steve Jobs kuzindua iPhone ya kwanza mnamo 2007.
Hata hivyo, thamani yake ilishuka kidogo kutoka kwa hatua hiyo muhimu, hadi kumaliza kikao cha biashara cha Jumatatu huko New York kwa $2.99tn.
Apple imekuwa mmoja wa washindi wakubwa wa janga hili, kwani athari za amri ya kutotoka nje iliyosabbaishwa na virusi vya corona ilifanya matumizi ya vifaa vya rununu kuongezeka.