Baada ya kukimbizwa hospitali Sadio Mane na Dias wako sawa

0

 

Nahodha wa Senegal Sadio Mane pamoja na golikipa wa Cape Verde Josimar Dias wote wanaendelea vizuri baada ya kukimbizwa hospitali kufuatia tukio la kugongana vichwa wakati wa mchezo wa 16 bora wa AFCON 2021 uliyomalizika kwa Senegal kushinda 2-0.

Josimar alioneshwa kadi nyekundu baada ya tukio hilo kutokea dakika ya 57, Mane aliendelea kucheza hadi dakika ya 63 akafunga goli ila dakika ya 70 akashindwa kuendelea na kukimbizwa hospitali.

Baada ya ushindi huo sasa Senegal wanafuzu kucheza hatua ya robo fainali ya AFCON 2021 na mshindi wa mchezo wa 16 bora wa Mali dhidi ya Equatorial Guinea ndio atacheza nae hatua ya robo fainali ya AFCON 2021.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable