Hata dakika 60 hazikupita, wakati urais wa Pedro Lascurain Paredes tayari ulikuwa historia.
Mwanasiasa huyo wa Mexico alikua rais wa Mexico mnamo mwaka 1913, na baada ya robo tatu ya saa aliwasilisha kujiuzulu kwake kwa bunge la Congress.
Huu ni muhula mfupi zaidi wa urais katika historia na hata umesajiliwa kwa njia hii katika Kitabu cha kumbukumbu cha Guinness.
Kwa miongo kadhaa, sura ya Lascurain imekuwa na tuhuma ya kuwa katika huduma ya mapinduzi ya kijeshi, na pia kwa jina la utani la "rais anayekimbia".
Lakini uchunguzi juu ya kile kilichotokea Februari 1913 unaonyesha jinsi mwanasiasa mwenye elimu nzuri, lakini uzoefu mdogo wa kisiasa, alivyoathiriwa na migogoro isiyotabirika ya Mapinduzi ya Mexico kati ya mwaka (1910-1920).
"Anajulikana katika historia kwa muda wake wa dakika 45 madarakani, rais wa muda mfupi zaidi kuwahi kuwepo. Hata hivyo, hakuna anayeangalia utendaji wake kama kansela," mwanahistoria Graziella Altamirano anaiambia BBC Mundo.
"Alichukua jukumu muhimu sana wakati mgumu wa uhusiano na Marekani, na mmoja wa mabalozi wabaya zaidi wa Marekani ambaye Mexico imekuwa naye katika historia yake: Henry Lane Wilson,"
Jinsi alivyokuja kukalia kiti cha urais wa Mexico kwa dakika 45 inaonyesha usaliti ambao uilimtesa Lascuraini kila mara.
"Ni unyanyapaa ambao haukutoweka na baada ya kipindi hicho alitumia miaka mingi kujaribu kueleza kilichotokea , kwa sababu kila mtu alimwambia alikuwa msaliti," anasema mwanahistoria Guadalupe Villa, mtafiti mwingine. ambaye amechunguza historia ya rais hiyo".
Siku kumi za kutisha
Kipindi kifupi sana cha urais wa Pedro Lascurain kilifanyika katikati ya siku 10 zenye wasiwasi - kuanzia Februari 9 hadi 19, mwaka 1913 - ambapo mapinduzi yalifanywa dhidi ya Rais Francisco I. Madero.
Tukio hilo linajulikana kama Muongo wa Kutisha.
Mwaka huo, Madero alikabiliwa na uasi wa kijeshi dhidi ya serikali yake, ambayo ilikuwa ya kwanza kuchaguliwa kidemokrasia baada ya miaka 30 ya utawala wa kijeshi wa Jenerali Porfirio DÃaz.
Lascurain, kama Waziri wa Mashauri ya Kigeni, alilazimika kukabiliana na shinikizo hizi kutoka kwa Wilson, ambaye hata alitaka wazi kujiuzulu kwa rais na kutishia kuandaa uingiliaji wa kijeshi wa Marekani huko Washington.
"Jukumu lake kama waziri wa mambo ya nje lilikuwa muhimu zaidi, kwa sababu ilikuwa wakati wa vitisho ambavyo Mexico imepata katika historia yake," anaelezea Altamirano.
"Mara kadhaa kulikuwa na hata meli kadhaa zilizowekwa, katika Pasifiki na katika Ghuba, kuzuia kila kitu kilichokuwa kikifanyika na kile ambacho Marekani ilitaka wakati huo," anaongeza.
Mexico ilikuwa imepoteza zaidi ya nusu ya eneo lake kwa nchi jirani miongo michache iliyopita, hivyo vitisho vya Marekani vilichukuliwa kwa uzito mkubwa.
Dakika zake 45 maarufu za urais
Jenerali Victoriano Huerta, ambaye Madero alimtumia kudhibiti uasi huo, hakuwa mshirika wa rais wake.
Kama ilivyojulikana baadaye, alikula njama na Jenerali Félix DÃaz (mpwa wa Rais wa zamani Porfirio DÃaz) na Balozi Wilson kumpindua Madero na kuchukua madaraka "kwa muda."
Waliuita "Mkataba wa Ubalozi".
Ili kufikia malengo yake, Lascurain "alitumiwa" bila uelewa wake.
Na ni kwamba mnamo Februari 18, 1913, katikati ya mapigano kati ya wafuasi watiifu na waasi, Madero na makamu wake wa rais, José MarÃa Pino Suárez, walikamatwa na vikosi vya Huerta.
Akiwa na hakika kwamba kila kitu kilikuwa kinyume chake na anguko lake lilikuwa karibu, siku iliyofuata rais aliandika barua yake ya kujiuzulu na kuikabidhi kwa Waziri wa Mambo ya Nje Lascurain ili kuipeleka kwenye Bunge la Congress.
Kwa upande wao waliomba njia salama wa kuondoka nchini.
"Maisha ya Madero tayari yalikuwa yameathirika, kama ya Pino Suárez. Tangu mwanzo walihukumiwa kifo, ingawa kulikuwa na ahadi kutoka kwa Victoriano Huerta," anasema Villa.
Lascurain alihutubia Bunge na barua ya Madero ya kujiuzulu na baada ya kuiwasilisha, kama katiba ilisema wakati huo, ilikuwa juu yake kuchukua serikali.
Hivyo ilikuwa kwamba Lascurain akawa rais.
Kwa kuamini makubaliano na Huerta, Lascurain alimteua mkuu wa waasi kuwa Katibu wa Mambo ya Ndani (afisa anayefuata katika safu ya "urithi") na kukabidhi barua yake ya kujiuzulu ndani ya dakika 45.
Kwa hivyo, Huerta alikuwa rais mpya.
Hapakuwa na njia salama au dhamana kwa uhamisho wa Madero na wenzake.
Yeye na Pino Suárez waliuawa mnamo Februari 22 nje ya gereza la Lecumberri, katika kisa kilichotajwa kuwa jaribio la kutoroka.
Msaliti?
Lascurain alijua hali aliyokuwa nayo tangu alipoandika barua yake ya kujiuzulu.
"Matukio tunayoshuhudia yameniweka katika nafasi ya kuwezesha njia za kutatua ndani ya sheria hali ambayo ingeweza kukomesha uwepo wa taifa," alisema wakati akizungumzia tishio la uvamizi wa Marekani.

Chanzo cha picha, Getty Images
Lakini hati ambazo Altamirano amepata zinaonyesha jinsi rais wa muda mfupi wa Mexico alijua kuwa ameanguka kutoka kwa neema.
"Lascurain anafika nyumbani kwake akiwa amekata tamaa, akaandika barua kwa mkono wake mwenyewe, niliona akisema, 'Nilidanganywa kabisa, mimi ambaye kwa nia njema nilitaka kumnusuru rais na makamu wa rais, walinidanganya kabisa '" Altamirano anaelezea.
"Wapo wanaosema hakupaswa kujiuzulu, lakini Chumba kilizingirwa na askari, alitishiwa, manaibu walikuwa tayari wamebeba kalamu mkononi kupokea kujiuzulu na dakika zao za kushika wadhifa wa urais kisha wajiuzulu. Kila kitu kilikuwa tayari na silaha. "
Baada kukimbilia uhamishoni nje ya nchi, Lascurain alirudi Mexico na alitumia miaka yake mingi akijaribu kusafisha jina lake.
"Labda alikuwa mjinga kidogo, kwa sababu aliamini alichoambiwa na wengine. Ili uwe mwanasiasa unahitaji kuwa na akili sana. Na hakuwa nayo."






