Mwimbaji, mwigizaji na mwanasiasa "Grand P" mwenye asili ya
Guinea, amemchumbia mpenzi wake wa muda mrefu EudoxieYao.
Grand p alichukua hatua hiyo ya kumchumbia mwanamitindoo huyo wa Instagram, ambapo wawili hao walikuwa wakifanya mahojiano kwenye kipindi cha mtangazaji Fanicko kwenye kituo cha Televisheni cha Gabon ndipo alipoamua kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake huyo wa kitambo.
Penzi hili limekua ni moja ya wapenzi maarufu zaidi huko Afrika ya Magharibi na limekua likichukua sifa nyingi na kujitokeza kwenye vichwa vya habari vyombo vingi vya utangazaji koteA frika