Mwanafunzi wa Nigeria auawa kufuatia madai ya kukashifu uislamu

0


 Ghasia zimezuka katika chuo cha elimu ya juu katika mji wa Sokoto kaskazini mwa Nigeria baada ya mwanafunzi wa kike wa Kikristo kudaiwa kutoa matamshi ya kashfa dhidi ya Uislamu.

Eneo hilo lina Waislamu wengi.

Wanafunzi wa Kiislamu katika Chuo cha Elimu cha Shehu Shagari wanaripotiwa kumuua msichana huyo na kuuchoma moto mwili wake.

Kisha wakaingia kwenye msako wa kuharibu mali yakiwemo magari.

Msemaji wa polisi katika jimbo la Sokoto aliambia BBC kuwa vikosi vya usalama viliingilia kati kurejesha hali ya utulivu na uchunguzi unaendelea.

Mamlaka imekifunga chuo hicho kwa muda usiojulikana na kuwaamuru wanafunzi kurudi nyumbani mara moja.

Kiongozi mkuu wa kidini wa Kiislamu nchini Nigeria, Sultan wa Sokoto, Sa'ad Abubakar, amelaani mauaji ya mwanafunzi huyo wa Kikristo na kuomba utulivu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable