#HABARI Chama cha Demokrasia na Maendeleo @chadematzofficial mkoa wa Mara, kimeiomba serikali kuangalia upya mifumo ya uendeshaji wa Shirika la Umeme (TANESCO) ili kudhibiti tatizo la umeme kukatika mara kwa mara.
Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Mara, Lucas Ngoto, ametoa rai hiyo na kusema mtanziko wa huduma ya umeme unaoshuhudiwa hivi sasa unapaswa kudhibitiwa haraka, ili kuepusha hasara ya kiuchumi inayoweza kurekodiwa.
#EastAfricaRadio
