Mohamed Salah alipotangaza kwamba ataondoka Liverpool mwishoni mwa msimu, Jürgen Klopp alimsifu kama "mmoja wa wachezaji bora wa wakati wote".
Kocha huyo wa zamani wa Reds alimuongoza katika taaluma yake kwa misimu yake mitano ya kwanza Anfield - ambapo Salah alifunga mabao 156, akishinda Ligi ya Mabingwa, Ligi Kuu, vikombe vitatu vya ndani, Kombe la Super Cup na Club World Cup. Kwa kweli ni mchezaji wa mpira wa miguu wa kipekee.
Lakini hiyo ni moja tu ya mambo mengi yaliomfanya kuwa ishara ya kimataifa na mfano wa kuigwa kwa watu walio mbali zaidi ya jiji la Liverpool, Uingereza, Ulaya, kote Afrika, kote katika ulimwengu wa Kiarabu na kwa Waislamu kila mahali.
Safari ya Salah inaonyesha kiwango cha kipekee cha kujitolea, uvumilivu na shauku.

Akiwa amekulia Nagrig, kijiji cha mbali nchini Misri, alianza taaluma yake huko Al Mokawloon Al Arab, akisafiri kwa basi kwa saa tisa kwa siku, kuanzia umri wa miaka 14, kwa ajili ya mafunzo huko Cairo.
Njia yake ya mafanikio imekuwa ngumu lakini Salah anakumbuka wakati ambapo kila kitu kilibadilika.
"Nilikuwa kwenye benchi kwa miezi miwili," aliambia Sports Illustrated. "Nilimwambia baba yangu, 'Siwezi kwenda... kila siku na kuwa kwenye benchi.' Nilikuwa nikilia. Alisema, 'Sikilizeni, kila mtu ambaye alitambulika baada ya muda mrefu, aliteseka sana [kwanza]. Haitakuwa rahisi. Endelea kuwa na malengo tu, fanya mazoezi kwa bidii na nina uhakika utacheza tena na kuwa bora.' Huo ni wakati ambao bado nakumbuka... Baada ya muda mfupi, nilianza kucheza tena - na kila kitu kimeenda sawa."
Lakini ilikuwa baada ya miaka kadhaa ya soka ya klabu ya Misri ndipo ujuzi wa Salah hatimaye ulimpeleka Ulaya, ambapo alisaini kujiunga na Basel, katika Ligi Kuu ya Uswisi.