Nimekuja hapa (Tanga) niwasalimie lakini kubwa niwape salamu za Rais, Rais anawasalimia sana na anawashukuru sana kwa kazi nzuri mliyofanya mwaka jana kurudisha Serikali ya CCM madarakani, Rais anasema tupo salama, tuchape kazi, twende vizuri,tujenge upendo na mshikamano wa Watanzania ili Taifa letu likuwe liwe na tija zaidi”- Mama Samia Suluhu, Makamu wa Rais wa Tanzania akiwa kwenye ziara Mkoani Tanga leo
