Star wa Mchezo wa mieleka @johncena amechukua hatua ya kuiomba msamaha China
Kauli hiyo imechukuliwa na kutafsiriwa kwenda kinyume au tofauti na taratibu zilizowekwa na mamlaka husika za sheria
Kitendo hicho kimefuata baada ya Star huyu kuinadi filamu aliyoshiriki ya Fast & Furious inayotarajiwa kuingia sokoni siku za hivi karibuni
Hivyo @johncena ali-tuma ujumbe wa msamaha kwa njia ya video kwenye mitandao ya kijamii kwa kuliomba radhi taifa la china kwa kile kilichotafsiriwa kuwa ni tofauti na kanuni kwa kuiita "Taiwan" ni nchi
"I love and respect Chinese. I am very sorry for my mistake. I am so sorry, I apologise" @johncena