#UNAAMBIWA: Wapo Watu wengi wenye umri mkubwa Duniani na na mmoja wao ni Bibi Kizee kutoka nchini Nepal

0

 


#UNAAMBIWA: Wapo Watu wengi wenye umri mkubwa Duniani na na mmoja wao ni Bibi Kizee kutoka nchini Nepal anayeitwa Batuli Lamichhane aliyezaliwa March 1903, kwa sasa ana Miaka 118 na bado anaonekana mwenye nguvu licha ya kuanza kuvuta sigara tangu akiwa na Miaka 17 (mwaka 1920) hadi leo.
Anapoulizwa swali la ni kwanini haachi sigara Batuli hujibu kuwa ———“Madaktari ambao tangu napata akili walinishauri nisivute sigara kwakuwa ni hatari kwa afya yangu wote wamefariki Dunia na Mimi bado nadunda kabisa, sasa kwanini niache kujipa raha kwa kuvuta!?”
Batuli huvuta sigara 30 kwa siku na anasema siri kubwa ya kuendelea kuwa na nguvu na mwenye afya licha ya umri wake ni kutoendekeza stress za ajabuajabu——-“Vijana wa sasa wana stress sana ndio maana hawaishi maisha marefu unatakiwa kujipa raha mwenyewe na kuwa na furaha wakati wote (no stress) hapo utaishi maisha marefu yenye afya tele”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable