Biden kufanya mazungumzo na magavana kuhusu moto wa nyikani

 

FILE - In this Sept. 14, 2020 file photo, Democratic presidential candidate and former Vice President Joe Biden speaks about climate change and wildfires affecting western states in Wilmington, Del. The United States is out of the Paris climate…

Rais Biden anafanya mazungumzo  na kundi la magavana kutoka majimbo manane ya Magharibi mwa Marekani

Rais wa Marekani Joe Biden anafanya mazungumzo Jumatano na kundi la magavana kutoka majimbo manane ya Magharibi mwa Marekani kuhusu kujiandaa na moto wa nyikani wakati eneo lote hilo linapambana na ukame.

Biden na maafisa wengine wa utawala watazungumza kutokea Ikulu na magavana kwa njia ya video.

Msemaji wa White House Jen Psaki aliwaambia waandishi wa habari wiki iliyopita mkutano huo utazingatia jinsi serikali kuu inavyoweza kuboresha matayarisho ya kupambana na moto wa nyikani na juhudi za kujibu, kulinda usalama wa umma, na kutoa msaada kwa watu wakati wa mahitaji ya haraka.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post