Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, limeidhinisha mkopo wa dola milioni 772 kwa Angola kama sehemu ya mpango wa miaka mitatu uliotiwa saini chini ya makubaliano yaliyofikiwa mnamo mwaka 2018 kwa lengo la kuleta mageuzi katika uchumi wa nchi hiyo. Fedha hizo zitatolewa mara moja katika jumla ya mkopo wa dola bilioni 3.7. Mkopo huo utatumika kuboresha utawala bora, mnyumbuko wa kiuchumi na kuendeleza uchumi soko utakaochepuliwa na sekta binfasi. Sambamba na kutoa fedha hizo, shirika la IMF limesema litaipa Angola muda wa hadi mwisho wa mwaka huu ili kuanza tena kulipa riba za mkopo wake.

