Jeshi la India lazuia kitisho cha shambulio Kashmir
Jeshi la India limesema limezuia kitisho kikubwa baada ya kuzizuwia ndege mbili zisizoendeshwa na rubani zilizokuwa zikiruka kwenye anga la eneo iliko kambi ya jeshi hilo katika jimbo la Kashmir. Tukio hilo limefanyika leo Jumatatu, siku moja baada ya ndege zisizokuwa na rubani zilizoshukiwa kubeba miripuko kutumiwa kushambulia kambi ya jeshi la anga katika eneo hilo linalozozaniwa kati ya India na Pakistan. Jeshi limesema wanajeshi walizigundua ndege mbili usiku wa manane zikiwa zinaruka katika anga la eneo la kambi ya kijeshi ya Kaluchak nje ya mji wa Jammu na kuchukua hatua ya haraka kuzilenga ndege hizo ambazo ziliondoka. Hakuna kundi la waasi lilitowa kauli yoyote kuhusu tukio hilo. Jimbo la Kashmir limegawika kati ya upande wa India na Pakistan na kila upande unadai liko chini ya himaya yake.
