Jeshi la Iraq lakosoa mashambulizi ya anga ya Marekani
Msemaji wa jeshi la Iraq amelaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani jana dhidi ya wanamgambo katika eneo la mpaka kati ya nchi hiyo ya Iraq na Syria. Msemaji huyo wa jeshi la Iraq, Yehia Rasool, amesema kitendo cha Marekani ni ukiukaji wa mamlaka ya nchi yake. Kauli ya ukosoaji ya Iraq ni ya nadra dhidi ya Marekani. Rasool aliandika ujumbe huo wa kuikosoa Marekani kwenye ukurasa wa Twitter baada ya mashambulizi ya Marekani kuua wapiganaji kiasi wanne wa kundi la kikosi cha wanamgambo wa Kishia wanaofungamana na Iran.
