Madatari wa Indonesia waambukizwa corona licha ya kuchomwa chanjo
Maafisa nchini Indonesia wamesema zaidi ya madaktari 350 wameambukizwa ugonjwa wa COVID 19, licha ya madaktari hao kuchomwa chanjo ya Sinovac. Madaktari wengine wengi wamelazwa hospitalini huku wasiwasi ukiendelea kujitokeza kuhusu ufanisi wa baadhi ya chanjo dhidi ya virusi vya corona na aina mpya ya virusi hivyo inayozidi kujitokeza. Badai Ismoyo, mkuu wa hospitali ya Kudus mjini Jarkata amesema madaktari wengi walioambukizwa hawakuwa na dalili zozote za corona na wengine walijiweka karantini, lakini wengine wengi walikuwa hospitalini humo wakiwa na homa kali na kupungua kwa viwango vyao kwa hewa ya Oksijeni. Hospitali hiyo inapambana na mripuko wa virusi hivyo unaosemekana kuchangiwa na aina mpya ya kirusi cha Delta.

