Hawa Mniga amekuwa mwanamke wa kwanza kuchukua fomu ya kuwania urais wa shirikisho la Soka Nchini Tanzania (TFF).
Hawa amechukua fomu hiyo ili kupambana rais wa TFF anayemaliza muda wake, Wallace Karia ambaye alichukua fomu ya kuwania tena nafasi hiyo Juni 8.
Mwanamke huyo ambaye ni mtumishi wa umma, alifika ofisi za TFF leo Ijumaa saa 11:00 asubuhi kisha kuingia moja kwa moja ndani kuchukua fomu.
Je unahisi Huu ni Muda wa Wanawake pia Kupewa Dhamana ya Kuongoza Soka la Tanzania..???

