Homebongo habariNaftali Bennett: Je, waziri mkuu mpya anayedaiwa kujivunia kuua waarabu atahusiana vipi na Wapalestina? Naftali Bennett: Je, waziri mkuu mpya anayedaiwa kujivunia kuua waarabu atahusiana vipi na Wapalestina? 0 ben June 14, 2021 CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGESMaelezo ya picha,Naftali Bennett amejitanabahisha kama mwanasiasa wa mrengo wa kushotoNaftali Bennett ameanza majukumu yake mapya kama Waziri Mkuu akiahidi kuliunganisha taifa hilo ambalo kisiasa lilikuwa katika mkwamo kwa kipindi cha miaka miwili.Wakati ikisubiriwa kuona kama atafanikiwa ama la kuitekeleza ahadi hiyo, suali kubwa linalomzunguka ni kwa namna gani atahusiana na Wapalestina.Kabla ya kuingia madarakani, Bw Bennet amekuwa ni mwanasiasa mwenye msimamo mkali dhidi ya Wapalestina na waarabu.Inadaiwa kuwa mwaka 2013 aliwahi kusema kuwa: " Nimeua waarabu wengi katika maisha yangu - na hakuna shida katika kufanya hivyo."Benett ambaye ni komando mstaafu wa jeshi la Israeli anaripotiwa kutasema maneno hayo katika maandamano ambayo yalikuwa yanapinga kuachiwa kwa wafungwa 104 kutoka kwenye jela za Israeli ili kuwezesha mazungumzo ya amani."Ukikamata magaidi, inabidi uwaue. Magaidi wanafaa wauawe si kuachiwa," inadaiwa mwanasiasa huyo wa mrengo wa kulia alisema.Benett pia anapigia chapuo kwa walowezi kuendelea kutwaa ardhi ya Wapalestina katika eneo la Ukingo wa Magharibi na Mashariki ya Jiji la Jerusalemu, eneo ambalo jumuiya ya kimataifa linaitambua kama ardhi ya Palestina.Benett pia haamini katika suluhisho la kuundwa kwa nchi mbili katika eneo hilo. Yaani dola la Israeli na dola la Wapalestina.CHANZO CHA PICHA,REUTERSMaelezo ya picha,Utawala wa Palestina hawategemei mapadiliko kutoka kwa utawala mpya wa Bennet"Nikiwa bado nina nguvu ya udhibiti wa jambo hili, siwezi kuiachia ardhi ya Israel," alisema hivyo katika mahojiano mwezi Februari 2021. Aidha bwana Bennett anahamasisha kuimarisha Israel kuendelea kushikilia ukingo wa magharibi - eneo ambalo wana mrengo wa kulia wananukuu katika biblia kwa jina la Judea na Samaria - kuwa ni lao.Je, mamlaka za Palestina zimepokea vipi utawala wa Benett?Viongozi wa makundi ya Palestina yametangaza kuwa hayatazamii kuboreshwa kwa mahusiano wa pande hizo mbili wakisema mabadiliko hayo ya uongozi yataendeleza siasa za mrengo wa kulia dhidi ya Palestina.Ofisi ya Rais wa Palestina Mahmoud Abbas imeeleza kuwa kura ya Jumapili "ni suala la ndani la Israeli," huku makundi yanayoongoza Ukanda wa Gaza wakiapa kuendelea kupigania haki za Wapalestina. Gaza imefungiwa kijeshi na Israeli katika maeneo yote kuanzia anga, ardhi na bahari toka mwaka 2007.Wizara ya Mambo Nje ya Palestina wakati huo huo imetoa taarifa yake ikisema "si sahihi" kuiita serikali ya muungano ya Bennett kuwa ni serikali ya mabadiliko labda kama kuna mabadiliko ya kisera juu ya suala la haki ya Wapalestina kujitawala na kuwa Jerusalemu Mashariki ni makao makuu ya Palestina."Ni kazi na taasisi ya kikoloni, ambayo tunapaswa kuipinga kwa nguvu ili kurudisha haki zetu," alisema msemaji wa Hamas, kundi la Kiislam linalodhibiti Gaza.Uhusiano wa Benett na Netanyahu upoje?Bennett, 49, aliwahi kuwa mshirika wake bwana Netanyahu, kwa kuwa mkuu wa wafanyakazi tangu mwaka 2006 mpaka 2008, wakati wawili hao walipokosana.CHANZO CHA PICHA,REUTERSMaelezo ya picha,Bennet na Netanyahu walikuwa washirika wakubwa wa kisiasa kabla ya kuchukua njia tofauti.Aliondoka chama cha bwana Netanyahu cha Likud party na kujiunga na mrengo wa pili katika chama cha taifa cha dini ya kiyahudi, na kuweza kuijngia bungeni baada ya kushinda uchaguzi wa mwaka 2013.Ameendelea kuwa waziri katika serikali zote za muungano mpaka mwaka 2019, wakati ambao chama chake kiliposhindwa kupata ushindi kwa mwaka huo.Lakini miezi kumi na moja baadae , bwana Bennett alifanikiwa kurejea bungeni kama kiongozi wa Yamina (waebrania wa mrengo wa kulia).Mara nyingi alionekana kuwa mzalendo, alikuwa anajitambulisha kama mtu wa mrengo wa kulia zaidi ya bwana Netanyahu), Naftali Bennett amekuwa anaongea waziwazi kuwa mtetezi wa Israel kama taifa la kiyahudi na katika historia ya Uyahudi na madai ya kidini katika kingo za magharibi, Mashariki mwa Yerusalemu na upande wa eneo la Syria -lililochukuliwa na Israeli tangu mwaka 1967 wakati wa vita vya mashariki ya kati. Tags bongo habari Newer Older