Nuru, Seth na Ezekiel wahukumiwa kunyongwa hadi kufa

0


Mahakama Kuu Kanda ya Kigoma imewatia hatiani washtakiwa Nuru Venevas, Seth Simon na Ezekiel Kalobezi kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa kosa la mauaji.

Imeelezwa mahakamani hapo mbele ya Jaji Matuma katika kesi ya mauaji Namba 36 ya mwaka 2020 kuwa mshtakiwa Nuru Venevas na wenzake wawili walifanya tukio hilo mnamo tarehe 2 Oktoba, 2016 majira ya usiku katika Kijiji cha Kwaga Wilaya ya Kasulu iliyopo Mkoani Kigoma ambapo walimvamia marehemu na walinzi wenzake wakiwa wanalinda mitambo ya kutengeneza barabara ya Kasulu-Kigoma na kumuua marehemu kwa kumkatakata na panga kisha kuiba control box ya excavator (sanduku la mchimbaji wa barabara) ambayo mshtakiwa Seth Simon alikamatwa nayo Mkoani Geita.

Hukumu hiyo ilitolewa mahakamani hapo baada ya ushahidi uliotolewa na Jamhuri pasipo kuacha shaka. na hivyo kupelekea washtakiwa wote watatu kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Kesi hiyo iliendeshwa na Mawakili wa Serikali Robert Magige na Edna Makala, ambapo upande wa utetezi uliongozwa na Sadick Aliki akiwa pamoja na Dennis Kayaga.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable