Wahudumu wa afya washambuliwa Afghanistan

0


Wafanyakazi watano wa huduma za afya nchini Afghanistan, waliopewa jukumu la kusimamia chanjo ya polio, walifariki kutokana na mashambulizi ya Taliban.

Taliban wanaendelea na mashambulizi yao dhidi ya wahusika wa mchakato wa chanjo, ambayo wanaona kama njama na watu wa Magharibi.

Wafanyikazi watano wa huduma ya afya walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa katika shambulizi dhidi ya timu ambayo ilikuwa ikiwajibika na chanjo ya polio katika mkoa wa Nangarhar.

Msemaji wa polisi wa jimbo la Nangarhar Farid Khan alisema kuwa wafanyakazi hao walipigwa risasi na kufariki katika maeneo matatu tofauti ndani ya masaa kadhaa.

Shughuli za chanjo katika mkoa huo zilisitishwa.

Taliban walikanusha madai ya kuhusika na shambulizi hilo.

Karibu miezi 3 iliyopita, maafisa 3 wa kike ambao walikuwa wakihudumu huko Jalalabad katika chanjo ya polio pia waliuawa.

Viongozi wa Taliban na viongozi wa kidini mara nyingi huwaambia jamii kuwa chanjo hizo ni njama za Magharibi za kuangamiza watoto wa Kiislamu, na pia wanashuku zinatumika kupeleleza shughuli za wapiganaji.

Maafisa wanasema Taliban hairuhusu kampeni za chanjo ya ndani katika maeneo wanayodhibiti.

Ramiz Alakbarov, Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan amelaani mashambulizi hayo.

Alakbarov alisema kwenye akaunti yake ya Twitter, "Kuwanyima watoto usalama wa maisha yenye afya sio unyama. Vurugu zisizo na maana lazima sasa zimalizike na wale waliohusika wanapaswa kuchunguzwa na kufikishwa mahakamani."

Balozi Mdogo wa Marekani Ross Wilson pia alidai kwamba vurugu za hivi karibuni zichunguzwe.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable