Home bongo habari Wanawake waishitaki tovuti ya video za ngono
Wanawake waishitaki tovuti ya video za ngono
ben
June 18, 2021
Zaidi ya wanawake 30 wameishtaki kampuni ambayo inamiliki tovuti ya kuonesha video za ngono kwa madai kuwa wametumiwa vibaya kwa kutumia picha zao za ngono.
Wanawake hao wanasema kuwa video zao ziliwekwa katika tovuti moja ya video za ngono bila idhini yao na wamewasilisha kesi mahakamani huko California.
Kesi hiyo inashutumu kampuni ya Mindgeek kwa kuendesha "biashara haramu".
Katika taarifa yake, tovuti hiyo na ngono ilitaja madai hayo kama ya "kusikitisha, ya kizembe na uwongo mtupu".
Tovuti za kuonesha picha za ngono zinatumiwa bila malipo lakini watumiaji wanaweza kulipa kwa mwezi ili kupata picha za ubora wa juu na maudhui mengine zaidi.
Na mara nyingi maudhui yake huwa ni ya watu wanaofuatilia mitandao hiyo na picha hizo huonekana na kila mmoja.
Hata hivyo, kampuni iliyoshitakiwa imesema kila video inayowekwa huwa inapitiwa tena na wasimamizi.
Tovuti hiyo ya ngono imeelezea BBC kuwa: "Haiwezi kabisa kuweka maudhui ambayo ni haramu na inachunguza malalamishi yoyote au madai yaliyotolewa juu ya maudhui yake kwenye jukwaa lao."
Ilisema kwamba "ina hakikisha usalama wa kutosha kwa watumiaji katika historia yake ikiwemo kupiga marufuku uwekaji wa maudhui ambayo hayajathibitishwa".
Hata hivyo, mshirika wa BBC nchini Marekani CBS, shirika hilo limesea kuwa tovuti za kuweka video za ngono hazihitaji watumiaji wake kuthibitisha utambulisho wao au umri kwa wale wanaoshiriki video hizo, kulingana na CBS, wala hazitafuti kuthibitisha idhini za watu wanaoshiriki video zinazowekwa kwenye tovuti zao.
Brown Rudnick LLP, kampuni ya sheria inayowakilisha walalamishi, imesema madai katika kesi hiyo yako chini ya ‘Sheria ya Ulinzi kwa Waathirika wa Usafirishaji haramu na Unyanyasaji ya mwaka 2000.’
Mmoja wa wanawake waliofungua kesi ameliambia shirika la CBS kwamba alikuwa na miaka 17 pekee pale mchumba wake alipomlazimisha kutengeneza video hiyo ya ngono.
Mwanamke huyo ambaye alitumia jina lisilo la kweli la Isabella, alisema video hiyo baadaye iliwekwa kwenye mtandao huo wa ngono bila idhini yake na yeye alijua hilo kutoka kwa rafiki yake.
Tovuti hiyo ya picha za ngono imesema "inachukulia kila malalamiko kuhusu utumiaji mbaya wa jukwaa lake kwa uzito mkubwa ikiwemo malalamiko katika kesi hii iliyowasilishwa mahakami".
Iliongeza kwamba haikuwa na nia ya kuacha "maneno yaliyotiwa chumvi katika kesi hiyo kutoonesha ukweli wa kuwa tovuti hiyo imeweka hatua na sera za kiusalama ambazo zinashinda za tovuti nyingine yoyote ile kubwa mtandaoni ".
Desemba mwaka jana, uchunguzi uliofanywa na gazeti la New York Times ulishutumu tovuti hiyo kwa "kutengeneza" video za unyanyasaji dhidi ya watoto na ubakaji – madai ambayo tovuti hiyo ilikanusha.
Mtandao huo ulisema kuwa ulitembelewa na watu bilioni 42 mwaka 2019, huku video milioni 6.83 zikiwekwa kwa muda jumla wa kutazamwa wa miaka 169 lakini haikusema ni wasimamizi wangapi iliajiri.