Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari apongeza kukamatwa kwa Nnamdi Kanu

 

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amevipongeza vyombo vya usalama na ujasusi kwa kumkamata kiongozi kundi lililopigwa marufuku la Biafra, Nnamdi Kanu na uvamizi wa nyumba ya mwanaharakati mashuhuri wa Yoruba, Sunday Adeyemo.

Ni mara ya kwanza rais amezungumza juu ya kukamatwa huko tata na kurudishwa Nigeria kwa kiongozi huyo anayetaka kujitenga kwa jimbo anakotoka .

Rais Buhari alizilimbikizia sifaidara za usalama nchini Nigeria kwa hatua hiyo .

mapu

Katika taarifa Bw Buhari alisema vyombo vya usalama vilionyesha umahiri mkubwa, uwezo na usiri katika kutekeleza oparesheni hizo Lakini hakusema mahali ambapo Nnamdi Kanu aliamatwa.

Bwana Buhari pia alipongeza uvamizi wenye utata wa makazi ya mwanaharakati maarufu wa yoruba Sunday Adeyemo ambapo kikosi maalum cha polisi kiliwaua watu.

Alimshutumu Adeyemo kwa kufanya vitendo vya ugaidi na kuvuruga amani kwa kisingizo cha kulinda haki za watu wake .

Wakati huo huo, Bunge la Uingereza linatarajiwa kuanza mjadala juu ya kumrudisha kiongozi wa ipob, Nnamdi Kanu kwenda Nigeria.

Katika ratiba iliyochapishwa kwenye tovuti yake, bunge lilisema litajadili hali iliyozingira kusafirishwa kwa Bw Kanu kwenda Nigeria kinyume na mapenzi yake miongoni mwa maswala mengine.

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post