Kuanzia Jumatano nchini Zimbabwe itasambazwa noti mpya ya dola 50, ikiwa ndio yenye thamani kubwa zaidi kuwahi kutolea Zimbabwe tangu mwaka 2019.
Dola 50 ya Zimbabwe ina thamani ya dola $0.60.
Noti mpya ilizunduliwa Jumanne na benki kuu ilisema kuwa itasambaza dola milioni 360 za Zimbabwe kupitia benki.
Imetolewa huku nchi hiyo ikikabiliwa na mfumuko wa bei ambao umewafanya watu kutembea lundo la noti.
Noti mpya ina picha ya shujaa wa kupambana na ukoloni Mbuya Nehanda.
Zim Live imetuma ujumbe wa twitter:
Tags
bongo habari