Takriban watu tisa, akiwemo mtoto mmoja, wamefariki kufuatia mafuriko na maporomoko ya udongo katika wilaya ya Kisoro kusini-magharibi ma Uganda.
Miili minane kati ya miili hiyo ilikuwa imefukuliwa kufikia Jumanne asubuhi, limesema Shrika la msalaba mwekundu la Uganda.
"Wa tisa ni mtoto ambaye aliangukiwa na udongo wakati alipokuwa akikimbia. Kwahiyo hakuna anayejua ni wapi hasa pa kuchimba ,"lilisema.
Mvua kubwa imeharibu nyumba, barabara, na miundo mbinu.
Jumatano, shirika la msalaba mwekundu lilisema kuwa linatoa msaada wa dharura kwa ajili ya familia 300 zilizoathiriwa na mkasa huo.
Awali shirika hilo lilituma picha kwenye Twitter , zilizoonyesha baadhi ya uharibifu:
