Mwanaume aliyekataa chanjo anyimwa tiba ya kupandikizwa moyo Marekani

0


 

Hospitali ya Marekani imemkataa kata kata mgonjwa aliyetaka kupewa matibabu ya kupandikiziwa moyo, kwasababu hakuchanjwa chanjo dhidi yaCovid-19.

DJ Ferguson, mwenye umri wa miaka 31, anahitaji sana moyo mpya, lakini hospitali ya Brigham and Women Hospital iliyoko Boston ilimuondoa kwenye orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa upasuaji huo, alisema baba yake, David.

Alisema kuwa chanjo ya Covidinakwenda kinyume na"kanuni za kimsingi za kijana wake, haiamini ".

Hospitali ilisema inafuata sera.

Hospitali ya Brigham and Womeniliiambia BBCkatika taarifa yake kwamba : "Ikizingatiwa upungufu uliopo wa viungo, tunafanya kila liwezekanalo kwamba mgonjwa anayepokea huduma ya kupandikizwa kiungo ana fursa kubwa ya kuishi."

Msemaji wake alisema hospitali inahitaji"Chanjo ya Covid-19, na mabadiliko ya mtindo wa maisha kwa wagonjwa wanaotarajiwa kupandikiziwa viungo vya mwili ili kuwa na uwezekano bora zaidi wa kufanikiwa kwa upasuaji na kunusurika kwa mgonjwa baada ya upandikizwaji, ikizingatiwa kuwa mfumo wa kinga mwili huwa unadhoofika haraka baada ya upasuaji ".

Hospitali hiyo iliongeza kuwa wengi wa watu 100,000 walioko katika orodha ya wale wanaosubiri kufanyiwa upandikizaji wa kiungo hawatapokea kiungo hicho katika kipindi cha miaka mitano kwasababu ya upungufu wa viungo vilivyopo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable