Waziri wa Utalii nchini Dkt.Damas Ndumbaro amesema kuwa katika soka la Afrika Simba hauwezi kuikosa kwenye 10 bora na ndio maana wakawapa tangazo la #VisitTanzania huku akidai pia wao kama Wizara walitamani Yanga isonge mbele katika mashindano yale sema ndo vile wakafungwa nje ndani
Dkt.Ndumbaro amesema
"Katika soka la Afrika Simba ni Brand,kwenye ligi yetu ya ndani hapa tunaweza kubishana lakini unakuja kwenye Afrika na unatakiwa uzitaje timu 10 bora Afrika au 12 au 20 basi lazima na Simba uitaje maana haiwezi kukosa pale.Na ndomaana tuliipa ile #VisitTanzania lakini hatukuwanyima Yanga tukawapa ile #VisitKilimanjaroAndZanzibar lakini wao wameenda mechi moja wamefungwa nyumbani na ugenini.Sisi kama wizara tulitamani Yanga iendelee ili lile tangazo lionekane onekane"
Na mwandishi wetu
@luckynaturebway
