Zelensky anasema anaweza kuzungumzana Putin- ila pasiwe na waamuzi

0

 

Rais wa Urusi Volodymyr Zelensky yuko tayari kuzungumza moja kwa moja na Rais wa Urusi Vradmir Putin, ila "pasiwepo na mtu mwingine yeyote wa kuwapatanisha", rai swa Ukraine ameiambia televisheni ya Italia , channel Rai 1.

Zelensky amesema anaweza kuzungumza tu na Putin, "kwa masharti ya mazungumzo, sio kwa kulazimishwa ".

Amesema "hatua ya kwanza ya wazi " ya kufanya mazungumzo inaweza kuwa wakati Urusi itakapoondoa vikosi vyake kutoka Ukraine.

Aliongeza kuwa ana kesi zaidi za '' ukatili wa wazi '' uliofanywa na warusi ambao ulionekana. kama ule uliofanyika katika Bucha , Borodyanka au Mariupol, jambo ambalo haliwezi kuvumiliwa katika mazungumzo yoyote na Warusi.

Ukraine na Urusi bado hazijafanya mazungumzo ya ana kwa ana tangu tarehe 29 machi na mpatanishi mkuu wa Moscow, Vladimir Medinsky, amekuwa akisema kuwa mazungumzo yalifanyika kwa njia isiyo ya ana kwa ana.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable