1. Utata kombe la dunia unaondoa ladha ya manshidano
Mwandishi wa michezo wa BBC, Gabby Logan anasema utata wa masuala mengi kuzunguka michuano ya mwaka huu ya kombe la dunia, inaondoa ladha na msisimko wa michuano hiyo.
Ukiukwaji wa haki za binadamu ikiwemo kuzuia mahusiano ya jinsia moja na kunyanyaswa kwa wafanyakazi wahamiaji nchini Qatar kama mwenyeji ni masuala yaliyochukua nafasi zaidi kuliko soka na michuano yenyewe.
2. England yapaa kwenda Qatar
Mwisho wa Twitter ujumbe, 1
Kikosi cha England kimeanza safari ya kwenda Qatar, kikiwana hari kubwa. England ni miongoni mwa mataifa yanayopigiwa chapuo kufanya vyema katika mashindano hayo baada ya miaka mingi ya kutoka kapa. Mara ya mwisho taifa hilo kutwaa kombe la dunia ilikuwa mwaka 1966.
3. Lennon astaafu soka
Wakati England ikijiandaa kwa ajili ya kombe la dunia, Aaron Lennon - aliyelichezea taifa hilo katika michuano ya mwaka 2006 na 2010 ametangaza kustaafu soka baada ya miaka 19.
Lennon aliitwa kwa mara ya kwanza na kocha Sven-Goran Eriksson kwenye kikosi cha England kilichoshiriki michuano ya mwaka 2006 huko Ujerumani akiwa na miaka 19, akachezea England mchezo wake wa kwanza dhidi ya Trinidad and Tobago.
Mwisho wa Twitter ujumbe, 2
4. Sitastaafu baada ya fainali za Qatar - Bale
Nahodha wa Wales, Gareth Bale amesema hafikirii kuachana na soka hata baada ya fainali za kombe la dunia huko Qatar zinazoanza Novemba 20, 2022.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 33, atakuwa na miaka 37 itakapofanyika fainali zingine, kama aliyonayo Christiano Ronaldo sasa anaye anakwenda kuiwakilisha Ureno huko Qatar.
Wales imeondoka leo, huku timu ya taifa ya mchezo wa Raga ikijipanga na kuwapigia makofi wachezaji hao wakiongozwa na Bale walipokuwa wanaondoka kwenda Qatar.
Mwisho wa Twitter ujumbe, 3
5. Ronaldo na Bruno Fernandes wasalimiana 'kitata'
Kiungo wa ortugal Joao Mario anasema kusalimiana kwa kupeana mkono kwa mashaka na kutazamana isivyo kawaida kati ya Cristiano Ronaldo na Bruno Fernandes siku ya Jumatatu, ilikuwa mzaha na "imetafsiriwa vibaya."
Kufuatia mahojiano ya Ronaldo na TalkTV, ambapo alisema alihisi "amesalitiwa" na Manchester United, sasa wengi walitaka kuona wachezaji hao wanaocheza pamoja United wakikutana watasalimianaje.
Salaam yao imeibua mjadala, kama Bruno kuonekana kutomtilia maanani Ronaldo, kama video inavyoonyesha.
Akizungumza na waandishi wa habari siku ya leo, Mario alisema: "Nilikuwa pale na niliona kila kitu, ilikuwa wakati wa kutaniana ambao ulitafsiriwa vibaya kwa nje.
Mwisho wa Twitter ujumbe, 4


