Baraza la Kiarabu lilitaka jumuiya ya kimataifa na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kukomesha adhabu ya kifo kwa Wamisri 12 waliopinga mapinduzi ikiwa ni pamoja na viongozi mashuhuri wa Ikhwanul Muslimin (Ikhwan).
Katika taarifa ya maandishi iliyotolewa na Baraza hilo likiongozwa na Rais wa zamani wa Tunisia Munsif al-Merzuki na kutetea haki ya watu wa Kiarabu kwa uchaguzi wa kidemokrasia, ilielezwa kuwa "maamuzi ya kushangaza" yaliyotolewa na mahakama ya Misri juu ya viongozi wa Ikhwan yalikemewa vikali .
Katika taarifa hiyo, jumuiya ya kimataifa na mashirika ya haki za kibinadamu waliombwa kuchukua hatua ili kuzuia utekelezwaji wa hukumu ya kifo.
