Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 23.07.2021: Kane, Mbappe, Pogba, Varane, Kessie, Hazard, Xhaka

Harry Kane

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Manchester City iko tayari kuwapoteza wachezaji kadhaa ili kuishawishi Tottenham kumuuza Harry Kane.

Manchester City wako tayari kumtoa mmoja wa wachezaji nyota akiwemo mshambuliaji wa Brazil Gabriel Jesus, 24, nahodha wa Algeria Riyad Mahrez, 30, kiungo wa Ureno Bernardo Silva, 26, au mshambuliaji wa Uingereza Raheem Sterling, 26, kama sehemu ya mpango wa kuishawishi Tottenham kuwauzia nahodha wa Uingereza Harry Kane. (FourFourTwo)

Kane atapokea kitita cha pauni 400,000-kwa-wiki atakapojiunga na Manchester City baada ya mwenyeiti wa Tottenham Daniel Levy kuidhinisha kuondoka kwake wiki iliyopita. (Sun)

Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 22, hatakubali mkataba mpya Paris St-Germain kwani anajiandaa kuhamia Real Madrid, licha ya klabu hiyo ya Ufaransa kutaka kumuunganisha na mchezaji mwenzake wa kimataifa Paul Pogba. (Marca - in Spanish)

Kylian Mbappe

CHANZO CHA PICHA,AFP

Maelezo ya picha,

Kylian Mbappe hana mpango wa kusaini mkataba mpya PSG

Pogba anatarajiwa kuondoka Manchester United msimu huu wa joto baada ya kukataa mkataba wa pauni milioni 350 kwa wiki licha ya klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Premia kutaka akamilishe mkataba wake wa sasa na kuondoka 2022. (Mirror)

Manchester United pia wanang'ang'ana kufikia makubaliana na Real Madrid kumsajili beki wa Ufaransa Raphael Varane, 28. Klabu hiyo ya La Liga inataka kulipwa £50m kumuachilia mlinzi huyo huku United wakiwa tayari kulipa £40m. (Mirror)

Liverpool ni miongoni mwa klabu kadhaa za Ulaya zinazotafakari uwezekano wa kumnunua kiungo wa kati wa AC Milan na timu ya taifa ya Ivory Coast Franck Kessie, 24. (Gazzetta dello Sport)

Kessie

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Kessie

Newcastle wana imani ya kumpata kiungo wa kati wa Southampton na Gabon Mario Lemina, 27, baada ya kufanya mazungumzo na wachezaji kadhaa wa safu ya kati ambao bei yao iko nje ya viwango vya mshahara wa klabu hiyo. (Northern Echo)

Eden Hazard, 30, tayari ameonesha wazi hisia zake kwamba kurejea kwake Chelsea haina mjadala baada ya vyombo vya habari vya Uhispania kuripoti kuwa Real Madrid inatafuta njia ya kumuuza. (Mirror)

Eden Hazard

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Eden Hazard asema kurejea kwake Chelsea haina mjadala

Arsenal imeambiwa na Sheffield United kuongeza ofa ya kumnunua Aaron Ramsdale ,32, kwa hadi pauni milioni 32 baada ya kukataa mara mbili dau la kumuuza kipa huyo. (Times - usajili unahitajika)

Chelsea pia wanamtaka kipa Muargentina Sergio Romero, 34, baada ya mkataba wake na Manchester United kukamilika,huku the Blues wakiendelea kumtafuta mchezaji wa tatu ambaye anaweza kushikilia nafasi ya Edouard Mendy na Kepa Arrizabalaga. (Telegraph - usajili unahitajika)

Granit Xhaka

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Xhaka amekuwa Arsenal tangu mwaka 2016

Kiungo wa kati wa Arsenal Granit Xhaka anakaribia kukamilisha uhamisho wake kwenda Roma baada ya klabu hiyo ya Serie A kuonesha ishara kwamba inamtaka ajiunge nao katika mechi ya kabla ya msimu huko Portugal wiki ijayo. (Daily Mail)

Aston Villa huenda wakawasilisha ofa ya kumnunua mshambuliaji wa River Plate na timu ya taifa ya Argentina Julian Alvarez wiki ijayo. (TNT Sports - in Spanish)

New Brentford signing Kristoffer Ajer celebrates scoring a goal for previous side Celtic

CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Kristoffer Ajer mlinzi wa Celtic aliyenyakuliwa na Brentford ya Norway

Mlinzi wa Tottenham na Marekani Cameron Carter-Vickers, 23, huenda akajiunga na Newcastle, ambao wanamtafuta mchezaji wa safu ya kati na nyuma baada ya Brentford kushinda kinyang'anyiro cha kumsajili mlinzi wa Celtic na timu ya taifa ya Norway Kristoffer Ajer, 23. (90Min)

Post a Comment

Please Select Embedded Mode To Show The Comment System.*

Previous Post Next Post