Lori zinazomilikiwa na raia wa Msumbiji zimeporwa na kuchomwa moto na waandamanaji katika nchi jirani ya Afrika Kusini, chama cha wasafirishaji mizigo Msumbiji kinasema.
Shirikisho la Chama cha Usafiri Barabarani (Fematro) linasema hakuna majeruhiwa au vifo vilivyoripotiwa miongoni mwa madereva.
Kisa hicho kilitokea mjini Durban, mkoa wa KwaZulu-Natal, ana kwengineko mkoani Gauteng, alisema Constantino Jotamo, mkurugenzi wa Fematro director.
"Tunatafuta maelezo zaidi kuhusu kile kilichotokea," alisema
Madereva wanahofia hali huenda ikaendelea kuwa mbaya zaidi katika siku zijazo.
"Siku chache zilizopita zimekuwa ngumu sana,” anasema Rui Muianga, dereva wa lori katika barbara ya Maputo-Johannesburg.
Siku ya Jumanne, ni magari matatu pekee ya usafiri wa umma ziliondoka Msumbiji hadi Afrika Kusini
