Rolf Buchholz raia wa Ujerumani ndiye mwanadamu ambaye mwaka 2010 alivunja rekodi ya dunia (Guiness World Record) ya kujiingizia vyuma vingi zaidi mwilini mwake (pini za vyuma) ambapo ndani ya mwili wake ana vipini 453 na tatoo zaidi ya 108.
Katika pini za vyuma zote hizo 453 vilivyopo mwilini mwake, pini 278 kati ya hzo zipo kwenye sehemu yake ya uzazi (uume), sasa unaweza kupata picha huyu ni mwanadamu wa namna gani mwenye pini 278 kwenye uume.
Mara nyingi Rolf Buchholz hutumia muonekano wake huo kujiingizia kupato kwakuwa amekua amekuwa na tabia ya kutembelea sehemu tofauti tofauti na kwenye matamasha na maonesho mbalimbali huku akiwataka watu walipe pesa kwa ajili ya kumshangaa.
