Na mwandishi wetu
Godson Mbilinyi
Fainali za michuano ya klabu Bingwa Barani Ulaya UEFA zimehamishwa kutoka jijini St. Petersburg nchini Urusi kwenda Paris Ufaransa kufuatia uvamizi wa Urusi kwa taifa la Ukraine.
Fainali hizo za michuano hiyo mikubwa duniani zilipaswa kufanyika Mei 28 nchini Urusi.
Katika mkutano wa leo wa viongozi wa UEFA wamekubaliana kuiondoa fainali ya michuano hiyo iliyopaswa kutimua vumbi kwenye dimba la Gazprom Arena na sasa itachapwa kwenye dimba la Stade da France in Paris kufuatia uvamizi wa Urusi kwa taifa la Ukraine.
