Mh.Jerry Muro ambaye aliwahi kuwa msemaji wa klabu ya Yanga na hivi sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi amesema kuwa anajua kabisa kuwa Haji Manara ambaye Sasa ndo msemaji wa Yanga amekuja katika klabu hiyo ili kutafuta ridhiki tu kwani Haji ni mwanachama damu wa klabu ya Simba
Mh.Jerry Muro amesema
"Ameanza tumpe muda naamini atafanya vizuri kama amekuja kwa nia ya dhati, na kama amekuja kwa hasira itatusaidia kutusogeza na pale hasira itakapoisha huenda akarudi alikotoka.Kila mtu anajua Haji ni do or die mwanachama wa Simba, Haji siyo mwanachama wa Yanga amekuja kutafuta riziki au mkate wake"
