Watu 10,000 watakaruhusiwa kutazama michezo ya Olympiki

0

 



Takriban watazamaji 10,000 ndio watakaoruhusiwa kuhudhuria Michezo ya 2020 Olympiki mjini Tokyo Japan, licha ya tahadhariya corona kutoka kwa wataalam wa afya.

Mashabiki kutoka nje ya nchi wamekwishazuiwa kuingia kwenye viwanja lakini waandaaji wanasema wakazi wataweza kufanya hivyo ili mradi hawazidi asilimia 50 ya idadi ya wanaopaswa kuwa uwanjani.

Mashabiki wanazuiwa kupiga kelelena watatakiwakutekeleza masharti kila mara wawapo viwanjani.

Michezo hiyo inatarajiwa kuanza tarehe 23 Julai huku Olympiki ya Walemavu- Paralympics ikitarajiwa -ikifuatia mwezi mmoja baadaye.

Waandalizi na serikali ya Japan wataoa tangazo kuhusu michezo ya Olympiki ya walemavu tarehe 16 Julai.

Hii inakuja baada ya wataalam wa afya kutoa ripori wakisema kuwa kuandaa shindano hiyo bila watazamaji na mashabiki "ni hatua itakayopunguza hatar "na wakatoa wito mashindano hayo yasiwe na watazamaji wala mashabiki viwanjani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable