Ndege ya abiria yapoteza mawasiliano angani na idara ya ufuatiliaji Urusi

0

 







Ndege ya Urusi iliyowabeba watu 28 imepoteza mawasiliano na idara inayofuatilia ndege angani katika rasi ya Kamchatka kusini mwa nchi hiyo.Msemaji wa idara ya uchukuzi Valentina Glazova ameliambia shirika la habari la AFP kwamba ndege hiyo aina ya An-26 ilikuwa ikisafiri kutoka mji mkuu wa rasi ya Kamchatka Petropavlovsk kuelekea mji wa bandarini Palana, wakati ilipotoweka na haikutua katika muda uliotarajiwa.Ameongeza kuwa ndege hiyo ilikuwa na jumla ya watu 28 miongoni mwao abiria 22 na wahudumu sita. Amesema shughuli ya kuitafuta ndege hiyo inaendelea.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable